DR.NDUGULILE: “WASANII IMBENI NYIMBO ZINAZOIHAMASISHA JAMII IACHE UOVU"

Na Mwandishi wetu, Arusha

Naibu Waziri wa Afya Dr Faustine Ndungulile amewataka wanamuziki wa Injili kuimba nyimbo zinazoweza kuihamasisha jamii kushiriki katika masuala mbalimbali ikiwamo uchangiaji wa damu salama.

Akizungumza wakati wa Tamasha la Tamani Festival lililoandaliwa na  Mtandao wa Wasanii wa Tansia ya Injili (Tagoane) Dk Ndungulile alisema yapo mambo mengi yanayohitaji ushiriki wa wasanii katika kukabiliana nayo.

" Yapo matukio yanawategemea wasanii mshiriki, imbeni nyimbo zinazoihamasisha jamii ipime magonjwa, iache uovu maana matukio ya kikatili nayo," alisema.

Dr Ndungulile ambaye ni muasisi wa uchangiaji wa damu nchini alisema uhai wa mama na mtoto pia unategemea uhakika wa damu salama.

Pia alikubali ombi la kuwa mlezi wa Tagoane akiahidi kushirikiana na wanamuziki kuhamasisha jamii kupima afya zao hasa wanaume ambao wengi hawashiriki.

Awali Rais wa Tagoane Dr Godwin  Maimu alisema taasisi hiyo imeamua kufanya tamasha la asante mama ili kuenzi mchango wa mwanamke katika jamii.

Pamoja na mambo mengine Tagoane walishiriki kufanya usafi katika hospitali ya Mount Meru na kuhamasisha uchangiaji wa damu salama.
 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile na Rais wa Tagoane wakutandika moja ya mashuka yaliyotolewa na Tagoane katika Hospitali ya Mount Meru Mkoani Arusha
DR.NDUGULILE: “WASANII IMBENI NYIMBO ZINAZOIHAMASISHA JAMII IACHE UOVU" DR.NDUGULILE: “WASANII IMBENI NYIMBO ZINAZOIHAMASISHA JAMII IACHE UOVU" Reviewed by Erasto Paul on July 01, 2018 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.