SHONZA: “SERIKALI ITAENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA VYAMA VYA WASANII”


Na Mwandishi wetu, Arusha


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza amesema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za vyama vya wasanii vinavyojikita katika mbalimbali zinazoleta maendeleo ya Taifa.

Shonza amesema hayo baada ya kushuhudia kazi zinazofanywa na Mtandao wa Tasnia ya Wasanii wa Muziki wa Injili Tanzania (TAGOANE) ikiwamo ya kuhamasisha jamii kuchangia damu salama ili kuokoa uhai wa mama na mtoto kupitia tamasha la Mama ni wa Thamani ( TAMANI FESTIVAL).

Akizungumza katika tamasha hilo jijini Arusha, Shonza alisema kazi ya sanaa sio tu kutoa burudani peke yake bali kuisadia jamii kuondokana na changamoto mbali mbali zinazowakabili.

" Tagoane ni kati ya taasisi makini za wasanii iliyoonyesha njia kwamba kumbe inawezekana kutumia burudani kuhamasisha jamii kuondokana na changamoto, ni wakati wa taasisi nyingine kuiga mfano huu," alisema.


Shonza alisema Serikali ipo tayari kufanya kazi na kuunga mkono vikundi vya wasanii vinavyoweza kutumia sanaa yake kuleta matokeo chanya kwa taifa.

Alisema tamasha la mama ni wa thamani linamuongezea heshima mwanamke wa kitanzania kwa kuwa ni ukweli usiopingika kuwa anao mchango mkubwa katika jamii yake.


Awali Rais wa Tagoane, Dk Godwin Maimu alisema wasanii wa injili waliamua kuandaa tamadha hilo kuenzi mchango wa wanawake wa kitanzania katika kupigania maendeleo ya taifa lao.

" Sekta ya afya inatuambia upungufu wa damu ni kati ya sababu za vifo vya wanawake wakati wa kujifungua, sasa katika kuitambua thamani ya mwanamke tumefungua kampeni ya kuchangia damu salama kuokoa uhai wa mama na mtoto," alisema.

Alisema kampeni hiyo itafanyika pia katika mikoa ya Manyara, Mbeya, Dar es Salaam na Dodoma na lengo kubwa ni kuihamasisha jamii kuvhangia damu salama.


Mbali na shughuli nyingine, TAGOANE walifanya usafi na kutoa msaada wa mashuka zaidi ya 400 kwa hospitali ya Mount Meru mkoani Arusha.


Baadhi ya wanamuziki wa muziki huo wa Injili walisema jukumu lao kubwa ni kuhakikisha wanahubiri neno la Mungu kwa njia ya uimbaji pamoja na kufanyia kazi kwa vitendo yale wanayoyaimba.

Mwisho.
SHONZA: “SERIKALI ITAENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA VYAMA VYA WASANII” SHONZA: “SERIKALI ITAENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA VYAMA VYA WASANII” Reviewed by Erasto Paul on July 02, 2018 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.