Kwa nini sitaki kushiriki tendo la ndoa na mume wangu?

https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/0125/production/_98139200_27b54018-f8b7-4443-8607-18ca0dab1604.jpg
Inaaminika kuwa asilimia 1 hadi 3 ya idadi ya watu hawana hisia zozote za kingono.

Kwa miaka kadhaa Stacey alishindwa kufumbua fumbo la ni kwa nini hakutaka kushiriki ngono na mtu yeyete hata mumewe.

Kama anavyoelezea hapa ni daktari wake aliyemwambia ukweli.
Kwa muda mrefu sana nilidhani nina matatizo ya kiakili na kiumbile.

Nilihisi kwamba sio jambo la kawaida kutoshiriki ngono.

Marafiki zangu wangezungumza kuhsu marafiki zao wa kiume ama hata watu maarufu ambao wangependa kushiriki nao ngono lakini mimi sikuwa na mtu yeyote akilini ambaye nahisi tungeshiriki naye ngono.

Wakati nilipokuwa katika miaka yangu ya ishirini nilianza kuona tofauti niliyo nayo , lakini singeweza kuambia mtu yeyote kwa sababu yalikuwa mawazo, watanifikiria mimi sio mtu wa kawaida, kwa hivyo nikaamua kunyamaza.

Kutokuwa na hisia zozote za ngono ACE sio jambo la kawaida ijapokuwa mara nyengine uhisi kuvutiwa ki-mahaba.

Nilikutana na mpenzi wangu ambaye sasa ni mume wangu wakati nilipokuwa na miaka 19, na sikujua maana ya kutokuwa na hisia za kushiriki ngono, hivyobasi nilidhani niko nyuma na kwamba sielewi mambo.

Nilikuwa nikifikiria kwamba nampenda sana mwanamume huyu na iwapo atanichumbia nitakubali asiliia 100 kwa sababu najua ningependa kutumikia maisha yangu yote naye, lakini kwa nini sitaki kushiriki naye ngono? ni jambo la kushangaza.

Tulizuru maeneo mbali mbali na aliniambia kwamba yeye atasubiri hadi siku ninayohisi kushiriki ngono naye.
Alinisaidia sana na hakutaka kunilazimisha kufanya kitu ambacho sikupendelea.

Nilifanya makosa makubwa kwa kutafuta katika mtandao sababu za kimatibabu ambazo husababisha mtu kutokuwa na hisia za kushiriki tendo la ngono.

Maadili ya kijamii yanaelezea kwamba ngono na watoto ndio sababu ya ndoa na marafiki zangu wote walikuwa wakiolewa na kupata watoto.

Nilifikiri mungu wangu kuna hili tarajio kwamba ninafaa kushiriki tendo la ngono na mumewe wangu ili kupata watoto.

Nilianza kuota ndoto za ajabu kwamba mumewe wangu huenda ataniwacha kwa msichana mwengine anayefanana nami lakini ambaye atakubali kulala naye na ikafikia kiwango ambacho wasiwasi wangu nilishindwa kuuvumilia.

Nilifikiria, wajua nini? ni muhimu kusuluhisha swala hilo , nilitaka kujua ni nini kilichokuwa kikiendelea, wakati huo nikiwa kati ya miaka 27 ama 28.

Nilifanya makosa ya kufanya utafiti katika mtandao na hayo yalikuwa makosa makubwa sana, kulikuwa na mambo mengi ambayo yalikuwa ya kawaida kama vile homoni zilizokuwa zikitoweka mara kwa mara , lakini kile ambacho niliiona ni kuwa na uvimbe katika ubongo.

Nilisema, mungu wangu nitafariki kutokana na uvimbe katika ubongo.

Nilienda kwa daktari wangu na kusema, tazama ni hatari?, nitafariki?

Aliniambia, tulia una tatizo la kutokuwa na hisia za kushiriki ngono.

Nilisema, ni nini hiyo? nini?
Sijawahi kuhisi kile watu wengi hutaja kuwa na hisia za kingono.

Hivyobasi alinielekeza katika mitandao na hapo ndipo nilipokutana na watu kama mimi.nilifurahi.
Sikuwahi kusikia kwamba kuna watu wasiokuwa na hisia za ngono.

Nilifanya utafiti zaidi na kuanza kujihisi kawaida, hivyobasi nilizungumza na mume wangu kuhusu swala hilo.

Na alisema, nilidhani kwamba kila kitu kilikuwa sawa .

Amekuwa mtu mzuri sana, amekuwa akinielewa sana.Baadhi ya watu walio na tatizo kama langu walikuwa na haya ya kusema:

Nina umri wa miaka 60 na sijawahi kukutana na mtu mwengine ambaye yuko kama mimi. Sijawahi kusikia hadharani .

Nilipotambua kwamba sina hisia za kushiriki ngono nilizungumza na watu kadhaa na huku wengine wakijitokeza na kuliangazia swala hili kwa uwazi nimepata majibu mabaya sana.

Kundi moja la wachezaji wenzagu katika chuo kikuu waliamua kunipangia kwenda kujiburidisha usiku kwa lengo la kutaka nishiriki ngono walipogundua kwamba sijashiriki ngono bila kujali kwamba nilikuwa na tatizo.

Kuna watu wengi wasio na hisia za ngono ambao wanapoanza uhusiano na mtu mwengine wanashiriki ngono na wanaendelea kama kawaida , lakini kwangu mimi kila wakati ninapokaribi kufanya tendo hilo mwili wangu unakataa kabisa.

Ni utoto mwingi na watu ninapowaambia hushangaa na kuniuliza ni vipi unaweza kupata watoto.

Ijapokuwa kuna njia nyingi za kupata watoto iwapo ninataka, ni swala ambalo linawezekana.

Nimegundua tatizo lango kwa miaka mitatu sasa.

Nasherehekea kuwa mtu mwenye tatizo hili, nafurahia na napenda kuzungumza na wengine ili watu zaidi kuelewa na sio kuwahukumu watu wasio na hisia za kufanya ngono.

Nadhani iwapo ningejua kwamba nina tatizo hili nilipokuwa na miaka 18 ama 19 nadhani afya yangu ya kiakili ingekuwa bora wakati mwingi wa miaka yangu ya 20.

La kushangaza zaidi ni kwamba wakati kabla ya kugundua tatizo langu mume wangu alikuwa akiniita Stace Ace
Kwa nini sitaki kushiriki tendo la ndoa na mume wangu? Kwa nini sitaki kushiriki tendo la ndoa na mume wangu? Reviewed by Erasto Paul on October 05, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.