Maji ya Mto Msimbazi hatari kwa viumbe hai


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2ylNZ2zrPRXnp5UKumwSVvYDlZ5cVe0X26pp63VNWj2E2hOTwf8u430HCG7Hw8fHPORB_eMGI9PIRM815kvsLVQ_0mos-7MwfC77giTA1eRhjCtNRJ4S9dnqGfUpLAvu5C8cHMtpt-bk/s1600/JANG1.jpg
Serikali imechukua sampuli ya maji ya Mto Msimbazi kwa ajili ya kuyachunguza ili kubaini kiwango cha sumu na ubora wa maji yake kwa matumizi ya binadamu.
 
Akitoa matokeo ya awali kwa wanahabari, Meneja wa  Maabara ya Mazingira  wa Ofisi ya Mkemia Mkuu, Emanuel Gwae, amesema kipimo cha maji ya Mto Msimbazi, katika eneo la Jangwani, kinaonyesha maji hayo yana kiwango cha oksijeni cha  milimita3.3.
Amesema kiwango hicho ni  kidogo na kwamba kinachohitajika ni kuanzia milimita sita.
“Hii inaonyesha namna ambavyo maji haya yamechafuka na viumbe hai waliomo humu hawawezi kuishi,” amesema Gwae.
Mchakato wa upimaji wa maji hayo umefanyika leo, Jumanne, Julai 11 katika tukio ambalo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina alilishuhudia.
Katika hatua nyingine, Ofisi ya Mkemia Mkuu ilichukua sampuli hiyo ya maji ambapo Waziri Mpina alishiriki kuchota maji hayo kwa ajili ya kupimwa.
Mbali na ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, wadau wengine waliokuwamo ni pamoja na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Bonde la Wami-Ruvu na Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC).
Mpina amesema kumekuwa na uchafuzi mkubwa katika Jiji la Dar es Salaam unaosababishwa na baadhi ya viwanda kutokuwa na mfumo wa kutibu maji taka na kusababisha maji yake kutitirika katika mito.
Amesema baada ya maji hayo kutiririshwa katika mito, matokeo yake ni kwamba mito inachafuka na kubadili rangi kutokana uchafu huo.
“Shughuli za umwagiliaji zinafanyika katika mito hii, sasa kwa kutazama tu haya maji yanakuwa na mchanganyiko wa kemikali hivi yakichanganywa katika vyakula hali itakuaje? Ndiyo maana tumeamua kuyachunguza ili kujiridhisha hali ipoje katika mito yetu,” amesema Mpina.
Mpina aliwataka wenye viwanda kuacha kutiririsha maji katika mito na kwamba watakaobainika watachukuliwa hatua  kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004.
Kwa mujibu wa Mpina pamoja na Mto Msimbazi, mito mingine minne iliyoathiriwa ni pamoja na Mlalakuwa, Ngo’mbe, Kijitonyama na Kibangu.
Mbali na sampuli hiyo, Mpina aliongoza mchakato wa kuyapima maji katika eneo la Jangwani ili kubaini kiwango cha oksijeni kilichomo kama ni sahihi kwa viumbe hai waliomo katika maji hayo kuishi.
 Mto Msimbazi unavyoonekana  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akiangalia kiasi  cha hewa ya Oxygen kilichopo katika maji ya Mto msimbazi akisaidiwa na
wataalamu kutoka katika maabara ya mkemia mkuu wa serikali hawapo  pichani, katika eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam leo. (Picha na  Evelyn Mkoko
Maji ya Mto Msimbazi hatari kwa viumbe hai Maji ya Mto Msimbazi hatari kwa viumbe hai Reviewed by Erasto Paul on July 11, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.