Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa ameeleza kuridhishwa na ujenzi wa daraja la Mto Lukuledi
lenye urefu wa mita 30.45 linalounganisha mikoa ya Lindi na Mtwara.
Amesema
ujenzi wa daraja hilo utakaogharimu Sh5.4 bilioni hadi kukamilika ni mkombozi
kwa wananchi wa mikoa hiyo na hasa wa wilaya za Ruangwa na Masasi.
Wananchi
hao wamekuwa wakishirikiana katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kilimo na
huduma za kijamii.
Waziri
Mkuu Majaliwa amesema hayo leo Julai 11, alipotembelea mradi huo katika Kijiji
cha Nandanga alipowasili wilayani Ruangwa akiwa katika siku ya pili ya ziara
yake ya kikazi ya siku nne mkoani Lindi.
“Watu
wengi wamepoteza maisha kwa kuliwa na mamba walipokuwa wakikatiza eneo hili.
Ujenzi wa daraja hili ni muhimu, watu wengi wa Ruangwa wanavuka kufuata
matibabu katika Hospitali ya Ndanda wilayani Masasi na wakazi wa Ndanda
wanavuka kufanya shughuli za kilimo wilayani Ruangwa,” amesema.
Waziri
Mkuu katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake amewaomba wananchi wa maeneo hayo
kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa mkandarasi anayejenga daraja hilo ili aweze
kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kumaliza kazi kwa wakati.
Mbunge wa
Ndanda, Cecil Mwambe amepongeza jitihada za Serikali za kuwaletea wananchi
maendeleo na kubadilisha maisha yao.
Amesema
mradi huo ni faraja kwa wananchi kwa kuwa eneo hilo ni makazi ya mamba, hivyo
kukamilika kwa ujenzi kutaokoa maisha ya watu na kurahisisha usafiri wa watu na
bidhaa.
Daraja Mto Lukuledi kuwaepusha wananchi kuliwa na mamba
Reviewed by Erasto Paul
on
July 11, 2017
Rating:
No comments:
Thank you for commenting to Mwanauswahili