Kabila la wala watu-3: Kumbe Mtoto wa Makamu wa Rais wa Aliliwa na Watu Hao

png-5_web
ENDELEA ILIPOISHIA: Uombaji radhi ulifanyika katika shughuli maalum iliyoandaliwa na viongozi wa Jimbo la East New Britaish na shughuli hiyo ilipewa jina la ‘reconciliation ceremony’ yaani sherehe ya maridhiano na ilifanyika Rabaul, mji mkuu wa jimbo  hilo ambalo lina wenyeji ambao ni wala watu.

“Katika kipindi hiki tumeguswa na kitendo kile na tunaomba msamaha na tunaamini leo tunafuta rekodi  hii (ya kuuawa kisha kuliwa kwa mchungaji na wenzake),” alisema Gavana wa jimbo hilo, Ratu Isoa Tikoca.

Ulaji wa watu ni kitu cha kawaida kwa watu wa sehemu za South Pacific , kwa mfano, Kisiwa cha Fiji kilikuwa kikijulikana kama Kisiwa cha Wala Watu na madazani ya wamisionari waliuawa eneo hilo na kuliwa na wenyeji wa hapo.

Mchungaji Brown  alikuwa anajua kwamba wenyeji wa visiwa vya Papua Newa Guinea ni wala watu. Aliwahi kuandika katika makabrash yake kwamba katika pitapita yake kisiwani humo akihubiri aliwahi kutembelea kijiji kimoja akakuta  mifupa 35 ya mataya, viganja vya binadamu ikiwa imebanikwa  ikiwa kwenye moja ya vibanda kijijini hapo.

“Mikono ya binadamu iliyookwa niliikuta ikiwa inaning’inizwa katika moja vibanda kijijini, nje kulikuwa na mnazi ambao ulikuwa na alama 76 ambazo wenyeji walituambia kila alama inawakilisha mtu mmoja aliyepikwa nyama yake na kuliwa hapa,” alisema Mchungaji Brown enzi za uhai wake alipokuwa akiwaambia viongozi wa Taasisi ya Royal Geographical Society.

Maneno hayo aliambiwa akiwa hajui kwamba wamisionari wenzake wa dhehebu la Methodist aliokuwa nao, tayari nao wameliwa huko alikowatuma kuhubiri na alipojua, aliingiwa na wasiwasi mkubwa juu ya maisha yake.
final-west-papua-jungle-indonesiadf3d8m-1680x1050
“Waliuawa na kuliwa kwa sababu tu, walikuwa wageni na wenyeji waliofanya hivyo hawakuwa na sababu nyingine isipokuwa walikuwa na tamaa ya kula nyama zao na kuchukua baadhi ya mali chache walizokuwa nazo,” aliandika Mchungaji Brown.

Kulitokea vurugu kati ya wenyeji na Wazungu kutoka Ulaya baada ya kitendo cha kuliwa watu hao weupe kwani vijiji kadhaa vilichomwa moto na mitumbwi ya wenyeji iliharibiwa. 

Makabila kumi ya visiwa hivyo yalilaumiwa kwa kushambulia wazungu na kuwala nyama hasa katika eneo linaloitwa Blanche Bay. Mchungaji Brown aliandika barua kwa Katibu Mkuu wa London Missionary Society aliandika hivi kabla ya kujua kuwa naye alikuwa

Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan akiongea na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe  Magufuli katika kongamano la wawekezaji wa Tanzania na Uturuki katika ukumbi wa BoT jijini Dar es salaam  jana Januari  23, 2017 ambapo wamesaini mikataba 9 ikiwemo ya sekta ya anga, elimu, utafiti n.k.

KARIBU TANZANIA
akiwindwa aliwe: “ Wenyeji wanatu-heshimu kuliko mwanzo, hii ni kwa sababu wanajua haki tuliyonayo inayotuumiza mioyo ya kuwaelimisha.” Hata hivyo, kuna taarifa kuwa Michael Rockefeller (pichani), aliyekuwa mtoto wa Makamu wa Rais wa Marekani, Nelson Rockefeller mwaka 1961  naye aliuawa na kuliwa nyama yake na watu hao. Ilikuwaje? Fuatilia Jumanne ijayo uone yaliyompata.

Basi hili linafanya safari kutoka Wilaya ya Kilolo vijijini huko Lulanzi kuja Iringa mjini kila siku na kurudi.

Yani basi limetoka huko masafa marefu tena katika njia mbaya sana zenye utelezi na mvua isiyokwisha,lkn ajabu linakuja kudondoka linapoingia mjin!! Vifo na majeruhi ni wengi.

Eeeh Mwenyezi Mungu zilaze Roho za marehem pema peponi na uwajaalie majeruhi wote kupona haraka, Amen.
Kabila la wala watu-3: Kumbe Mtoto wa Makamu wa Rais wa Aliliwa na Watu Hao Kabila la wala watu-3: Kumbe Mtoto wa Makamu wa Rais wa Aliliwa na Watu Hao Reviewed by Erasto Paul on January 24, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.