Uhali gani shoga yangu? Kiafya mwenzako kama ulivyoniacha jana, kama ni
mzima ni jambo la kumshukuru lakini pia kwa wale wagonjwa nawaombea
Mwenyezi Mungu ataweka wepesi! Baada ya hayo, nigependa kuzungumza na
wewe shoga yangu kuhusu athari za kumwambia mumeo umechoka.
GPL
Najua unatoa macho na kushangaa! Shoga,
kuchoka ninakozungumzia si kule kwa kufanya kazi za nyumbani kama
kupika, kufua, kuuza duka, kuwa bize na watoto, hapana!
Shoga kilichonisukuma leo kuandika haya
ni mahususi kwa wenzetu walee ambao huwanyima waume zao chakula cha
usiku, najua nikisema chakula cha usiku umenipata shoga yangu, kama
hujanipata basi hapa patakuwa hapakuhusu, upo? Shoga hivi ujue kuna
wanawake wana kauli za ajabu kwa waume zao hasa ukifika muda wetu ule wa
chakula cha usiku.
Utasikia anadai kwamba amechoka hivyo
ahitaji kusumbuliwa, looo! Aibu! Ngoja niwaulize, hivi unapomwambia
mumeo kwamba umechoka na huwezi kumpa chakula cha usiku unafikiri nani
atakayempa chakula hicho?
Shoga, nafikiri unajua mtu anapokuwa na
njaa anahitaji nini ili hali yake iwe sawa, ni wazi kwamba anahitaji
chakula, akila utamuona anavyochangamka kwa furaha, umeona enhh!
Hiyo ni njaa ya kawaida, sasa inakuwaje
kwa yule mwanaume mwenye hamu ya mambo yetu yalee, anayekuwa amemmisi
sana mkewe na kuhitaji kupata naye chakula cha usiku halafu mkewe
amwambie amechoka na hajisikii.
Bila shaka, atanyong’onyea na ni rahisi
kuamua kuitafuta shibe hiyo kwa wanawake wa nje wanaoweza kuwapa chakula
hicho bila masharti tena kikienda sambamba na mapochopocho kibao,
umenipata shoga!
Wakati mwingine sikatai, inawezekana ni
kweli kuwa umechoshwa na majukumu ya nyumbani au ofisini, lakini ni
vyema kutumia lugha ya kujiongeza kumuelewesha mumeo ili akuelewe kuliko
kumwambia;
“Na wewe baba Jamal umezidi, kila siku
unataka, nimekwambia nimechoka, sitaki sasa!” Shoga kuna wengine
wanadiriki kuwaambia kwamba kama wamebanwa sana na njaa wakatafute
wanawake wa nje wanaoweza kuwapa chakula cha usiku kila siku.Shoga
yangu, hivi unaipenda ndoa yako kweli?
Hujui kama kauli za namna hiyo zinaweza
kuisambaratisha ndoa yako na mumeo kuamua kutafuta mtu mwingine mwenye
kauli nzuri za kujitetea inapotokea amechoka na mumewe kuhitaji chakula
cha usiku. Shoga nina mengi ya kuzungumza na wewe lakini kwa leo niishie
hapa.
GPL
Kwa nini uchoshwe na chakula cha usiku?
Reviewed by Erasto Paul
on
January 24, 2017
Rating:
No comments:
Thank you for commenting to Mwanauswahili