Mbunge Afukuzwa Kanisani kwa Kusema ana Virusi vya HIV


 kasune-portrait
“Wakati niligundua kuwa nilikuwa na virusi vya HIV, nilijua kuwa nilikuwa na jukumu la kueneza habari kuhusu njia HIV unaweza kuambukizwa, unaweza kuzuiwa na pia njia za kumaliza unyanyapaa,” Kasume alisema.

Katika sehemu kubwa ya maisha yake, amethirika na virusi vya HIV. Alilelewa kijijini na aliwapoteza wazazi wake wote kwa ugonjwa wa ukimwi akiwa na umri wa miaka 14 na kisha akaolewa akiwa na umri wa miaka 18.
Akiwa na ndoto na kuona kizazi kichajo kisicho na virusi vya ukimwi, uamuzi wake wa kutangaza hadharani hali yake ulizua tofauti kubwa.

Kanisa lake lilimtimua kwa kuchukua hatua hiyo na kwa kwenda kinyume na matakwa ya mmewe kuhusu kuweka siri hali yake ya kuishi na virusi vya ukimwi.

Amesafiri sehemu mbali mbali za dunia na kukutana na viongozi wakiwemo marais wa zamani nchini Marekani wakiwemo Bill Clinton na George W Bush pamoja na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon. Wakati mmoja akitoa hotuba, aliwakumbusha wabunge wenzake kuhusu umuhimu wa kupimwa hali zao.

GPL
Mbunge Afukuzwa Kanisani kwa Kusema ana Virusi vya HIV Mbunge Afukuzwa Kanisani kwa Kusema ana Virusi vya HIV Reviewed by Erasto Paul on December 01, 2016 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.