Majambazi Wavamia Mgahawa, Wapora na Kujeruhi Mwanza

WATU wanaodaiwa kuwa majambazi wamevamia mgahawa wa Dinners uliopo katika mtaa wa Kenyatta Road jijini Mwanza na kupora kiasi cha fedha kisichojulikana na kujeruhi watu wawili kwa risasi kabla ya kutoweka.
 http://globalpublishers.co.tz/wp-content/uploads/2016/12/Kamanda-wa-Polisi-Mkoa-wa-Mwanza-Ahmed-Msangi.jpg
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, majambazi hao wanadaiwa kuingia ndani ya mgahawa huo majira ya jana alasiri na kufyatua risasi kadhaa kutoka ndani ya mgahawa huo.

Tukio hio limetokea katika eneo ambalo limezungukwa na taasisi za kibenki ikiwemo benki ya NMB, Kenya Commercial Bank KCB na wakala wa benki ya CRDB na zote zikilindwa na askari ambao hawakuweza kutoa msaada wowote licha ya kuwa ndani ya mita 30 kutoka katika mgahawa huo.

Moja ya watu waliojeruhiwa alikuwa ni muuza mitumba nje ya mgahawa huo na mwingine akiwa na asili ya Asia ambaye haijajulikana alikuwa nani katika mgahawa huo.

Akizungumza katika tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amekiri kuwepo kwa tukio hilo na kusema atazungumza na vyombo vya habari kesho (leo) baada ya kupata taarifa kamili.

Source;GPL
Majambazi Wavamia Mgahawa, Wapora na Kujeruhi Mwanza Majambazi Wavamia Mgahawa, Wapora na Kujeruhi Mwanza Reviewed by Erasto Paul on December 01, 2016 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.