Waziri wa maji na Umwagiliaji na Mbunge wa
 Jimbo la Wanging'ombe Mhandisi Gerson Lwenge Amemuagiza Mkuu wa Wilaya 
ya Wanging'ombe Kwenda Kufuatilia Malalamiko ya Wananchi wa Kata ya 
Uhambule Juu ya Madai ya Matumizi Mabaya ya Fedha za Ujenzi wa Kituo Cha
 Afya Cha Kata Hiyo.
Wakazi Hao Wametoa Malalamiko Hayo Wakati 
wa Ziara ya Mbunge wa Jimbo Hilo Mhandisi Gerson Lwenge Alipofika Katika
 Kijiji Cha Uhambule Kwa ajili ya Ziara ya Kutembelea na Kukagua 
Shughuli za Maendeleo na Kwamba Wanashindwa Kufahamu Ziwapi Fedha Zao 
Ambazo Walichanga Kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo Cha Afya.
Wamesema Walichangia Shilingi Milioni Nane
 Ambazo Zilipaswa Kutumika Katika Ujenzi wa Kituo Hicho Ambacho Hata 
Hivyo Kilivunjwa Kutokana na Kujengwa Chini ya Kiwango na Kuilazimu 
Halmashauri Kupeleka Fedha Nyingine Kwa ajili ya Ujenzi Huo.
Kutokana na Malalamiko Hayo Ambayo 
Yameonekana Kumtaka Waziri Lwenge Kuchukua Hatua Ngumu Juu ya Suala Hilo
 Amelazimika Kumuagiza Mkuu wa Wilaya Hiyo Mohamed Ally Kassinge 
Aliyewakilishwa na Katibu Tarafa Bi.Frola Nyato Kulifuatilia na Kumpa 
Taarifa Haraka Iwezekanavyo.
Mbunge Lwenge Amesema Haiwezekani Wananchi Wakachanga Fedha ZaoHalafu Zikatafunwa na Baadhi ya Viongozi Wabadhilifu Katika Serikali Hii Inayowapigania Wanyonge.
Hata Hivyo Amesema Endapo Kutabainika Kuwepo Kwa Udanganyifu Katika Fedha Hizo Basi Atatoa Maelekezo Kwa Mkuu Huyo wa Wilaya.
WAZIRI WA MAJI AMUAGIZA DC WANGING'OMBE KUFUATILIA UCHAKACHUAJI WA FEDHA ZA KITUO CHA AFYA 
 Reviewed by Erasto Paul
        on 
        
August 24, 2017
 
        Rating:
 
        Reviewed by Erasto Paul
        on 
        
August 24, 2017
 
        Rating: 
       
 
No comments:
Thank you for commenting to Mwanauswahili