WAZIRI WA MAJI AMUAGIZA DC WANGING'OMBE KUFUATILIA UCHAKACHUAJI WA FEDHA ZA KITUO CHA AFYA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwjCg6Lyk-jVIn-iUBoi4j9rfpRouP8IdnYri8LRq3ny2LfAe1IcuMzocH51pmjIMagybkFwuj-ZONAi_wuQKDeaUAMfLikcGBkJqgkRT7vSJ2Y0BJCr4Gn9rfpQxG9HBIXfZ08Njm3J8/s640/P1150392.JPG
 
Waziri wa maji na Umwagiliaji na Mbunge wa Jimbo la Wanging'ombe Mhandisi Gerson Lwenge Amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Kwenda Kufuatilia Malalamiko ya Wananchi wa Kata ya Uhambule Juu ya Madai ya Matumizi Mabaya ya Fedha za Ujenzi wa Kituo Cha Afya Cha Kata Hiyo.
Wakazi Hao Wametoa Malalamiko Hayo Wakati wa Ziara ya Mbunge wa Jimbo Hilo Mhandisi Gerson Lwenge Alipofika Katika Kijiji Cha Uhambule Kwa ajili ya Ziara ya Kutembelea na Kukagua Shughuli za Maendeleo na Kwamba Wanashindwa Kufahamu Ziwapi Fedha Zao Ambazo Walichanga Kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo Cha Afya.
Wamesema Walichangia Shilingi Milioni Nane Ambazo Zilipaswa Kutumika Katika Ujenzi wa Kituo Hicho Ambacho Hata Hivyo Kilivunjwa Kutokana na Kujengwa Chini ya Kiwango na Kuilazimu Halmashauri Kupeleka Fedha Nyingine Kwa ajili ya Ujenzi Huo.
Kutokana na Malalamiko Hayo Ambayo Yameonekana Kumtaka Waziri Lwenge Kuchukua Hatua Ngumu Juu ya Suala Hilo Amelazimika Kumuagiza Mkuu wa Wilaya Hiyo Mohamed Ally Kassinge Aliyewakilishwa na Katibu Tarafa Bi.Frola Nyato Kulifuatilia na Kumpa Taarifa Haraka Iwezekanavyo.
Mbunge Lwenge Amesema Haiwezekani Wananchi Wakachanga Fedha ZaoHalafu Zikatafunwa na Baadhi ya Viongozi Wabadhilifu Katika Serikali Hii Inayowapigania Wanyonge.
Hata Hivyo Amesema Endapo Kutabainika Kuwepo Kwa Udanganyifu Katika Fedha Hizo Basi Atatoa Maelekezo Kwa Mkuu Huyo wa Wilaya.
WAZIRI WA MAJI AMUAGIZA DC WANGING'OMBE KUFUATILIA UCHAKACHUAJI WA FEDHA ZA KITUO CHA AFYA WAZIRI WA MAJI AMUAGIZA DC WANGING'OMBE KUFUATILIA UCHAKACHUAJI WA FEDHA ZA KITUO CHA AFYA Reviewed by Erasto Paul on August 24, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.