Mwanamitindo na Mbunifu wa Mavazi Kutoka Njombe.

Anaitwa Sakina Emmanuel (20)  jina la sanaa ni Skyler,ni Mwanachuo  akisomea Sanaa ya Uandishi wa habari  na Utangazaji katika chuo kimoja kilichopo Mjini Njombe.
Licha ya kukabiliwa na masomo hayo ya sanaa pia ni mwanamitindo anayechipukia kutoka  Mkoa wa Njombe.
Tayari kazi yake ya kubuni mavazi imeshaanza kuonekana kwani baadhi ya wananchi Mjini Njombe wameshaanza kutumia bidhaa anazozalisha kwa mikono yake.
Umri wake wa miaka 20 unaonekana ni mdogo ukilinganisha na mipango mikubwa aliyonayo.
Sakina anasema anatamani kuona ndoto yake ya kuifikia jamii kwa kiwango kikubwa inafakiwa kwani sio kupitia sanaa pekee lakini pia anampango wa kuwatembelea wanafunzi wa kike katika shule mbalimbali za Sekondari zinazopatikana katika Mji wa Njombe akiwa na lengo la kupiga nao story na kuwaeleza namna gani wanaweza kufikia maelengo yao.
Anasema watoto wakike wanakabiliwa na matatizo mengi kutokana na uwepo wa wanafunzi wengi waliokosa semina elekezi juu ya Elimu Rika katika maswala ya Matumizi ya Pedi wakati wa kujisitiri katika mizunguko ya siku za Hedhi.
Sakina tayari ameshaanza kufanya harakati za kupata vibali vya kufanya shughuli hiyo  kutoka mamlaka za Serikali huku changamoto kubwa inayomkabili ni kukosa  ufadhili.
Hivi Karibuni Bi Sakina akiwa katika Kipindi cha Kachumbari  kinachorushwa na kituo cha Redio Kings Fm alisikika akieleza dhamira yake ya kweli juu ya namna atakavyofanikiwa mpango huo wa kuisaidia jamii.
Anasema japo hataweza kutoa misaada ya kifedha lakini anaamini ujumbe kupitia elimu anayotarajia kuitoa utakuwa na chachu hata katika masomo ya wananfunzi hao wa kike.
Katika mahojiano na kituo hicho pia aliwaomba wadau na wale watakaoguswa kumuunga mkono katika kufanikisha malengo yake.

Picha hapa chini zinamuonyesha  akiwa amevalia baadhi ya Mavazi aliyobuni Yeye Mwenyewe.
Image may contain: 1 person
No automatic alt text available.
Image may contain: 1 person
Image may contain: 1 person, shoes
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, smiling, shoes and text
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, standing and text
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, standing
Image may contain: 1 person, smiling, shoes and text
Mwandishi;Erasto Mgeni.
Mwanamitindo na Mbunifu wa Mavazi Kutoka Njombe. Mwanamitindo na Mbunifu wa Mavazi  Kutoka Njombe. Reviewed by Erasto Paul on August 23, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.