Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ametembelea na kuzindua nyumba ya wahudumu wa afya katika kijiji cha Mkungo wilayani Chato mkoani Geita zilizojengwa na taasisi ya Mkapa Foundation kwa kushirikiana na Serikali.
Akizindua
nyumba hizo, Rais Mkapa aliwasalimia wanachi kwa salam yake ya “mambo” na
wananchi kuitika poa” na kuwataka kutunza nyumba hizo na kushirikiana vema na
watumishi watakaoshi katika nyumba hizo kisha msafara wake kuondoka na kuelekea
Ikulu ndogo iliyopo Chato.
Mkapa
aliingia katika eneo la zahanati hiyo saa sita mchana akiongozana na mkewe,
Mama Anna Mkapa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.
Uzinduzi
wa nyumba hiyo ni ishara ya kuzindua nyumba nyingine 50 zilizopo katika mikoa
ya Geita, Simuyu na Kagera .
Makabidhiano
ya nyumba hizo yanatarajiwa kufanyika kesho (leo) katika uwanja wa mpira wa
miguu uliopo Chato mjini hafla itakayohudhuriwa na Rais John Magufuli.
Ofisa
Mahusiano na Mawasiliano wa Mkapa Foundation, Deogratius Rimoy alisema nyumba
50 zilizojengwa na taasisi hiyo katika mikoa mitatu tofauti zimegharimu kiasi
cha Sh 2.5 bilion
Amesema
lengo la kujenga nyumba hizo ni ili kuboresha huduma za afya vijijini illi
watumishi waweze kutoa huduma za afya kwa saa 24.
Mkapa atoa salamu ya ‘mambo’ akizindua nyumba za wahudumu wa afya Chato
Reviewed by Erasto Paul
on
July 09, 2017
Rating:
No comments:
Thank you for commenting to Mwanauswahili