Limao na barafu kwa kung’arisha ngozi

lemon
LEO kwenye safu hii tutaongelea jinsi ya kuifanya ngozi yako kuwa kavu na kung’aa kwa wale wenye mafuta kwa kutumia toner ya limao na barafu.

Mahitaji
Glasi ya maji
Limao
Kijiko
Tray ya barafu

JINSI YA KUPATA TONER HIYO
Chukua maji masafi, changanya na maji ya limao kisha koroga kuhakikisha limao na maji vimechanganyika. Baada ya hapo, weka maji hayo kwenye tray ya barafu kisha weka kwenye friji mpaka yagande.

Jinsi ya kutumia toner hii Unaweza kutumia baada ya kuoga, unachukua lile barafu lako lenye limao tayari, unasugua kwenye ngozi yako.

Kazi yake ni kufungua vitundu vya hewa na kung’arisha ngozi kwa ujumla. Tumia barafu hilo kabla ya kupaka makeup. Mbali na kufanya kazi hizo mbili, pia inasaidia kuifanya ngozi yako kubana.

Nikisema hivyo namaanisha inaepusha ngozi kulegea, nadhani tumewahi kuona ngozi ikilegea mpaka inaning’inia. Wengine hupenda kutumia toner hii usiku baada ya kutembea juani kwa muda mrefu na baada ya ngozi kuchoshwa na make-up za kila siku.
Limao na barafu kwa kung’arisha ngozi Limao na barafu kwa kung’arisha ngozi Reviewed by Erasto Paul on January 24, 2017 Rating: 5

No comments:

Thank you for commenting to Mwanauswahili

Powered by Blogger.